Barnabas Elias 'Barnaba Boy' akiwa na mama yake mzazi enzi za uhai wake. Mwanamuziki Barnabas Elias 'Barnaba Boy' alfajili ya jana (Jumamosi) aliondokewa na mama yake mzazi aliyekuwa anasumbuliwa na presha. Kupitia ukurasa wake wa Twitter muda mfupi uliopita Barnaba ameweka picha yake akiwa na marehemu mama yake enzi za uhai wake na kuandika ujumbe huu wa majonzi:
Amka. Mama hata dk.1 uliniita nikakwambia naja kesho kumbe ulikuwa uniage. Mama angu amka. Uwii nani ale matunda yangu. Ujumbe mwingine alioandika staa huyo kutoka kundi la THT ni huu:
Lala mahali pema peponi na Mungu akuweke kwenye amani ya milele. Naumia mama amka. Hata Dk. 1 uwiii. Umefanya niimbe leo. Haupo, uwii mama yangu!
Mtandao huu unamtakia roho ya ujasiri Barnaba katika kipindi hiki kigumu na Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu. AMEN.
TUPE MAONI YAKO HAPA:
0 comments:
Post a Comment